Mfungo wa Mitume
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mfungo wa Mitume (pia: Mfungo wa Mitume Watakatifu, Mfungo wa Petro na Paulo, Mfungo wa Mt. Petro na hata Mfungo wa Rafik) [1] ni mfungo unaofanywa na Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki na Wakatoliki wa Mashariki.
Mfungo huo unaanza Jumatatu ya pili baada ya Pentekoste (siku baada ya Jumapili ya Watakatifu Wote) na kuendelea hadi sikukuu ya Mitume Petro na Paulo inayoadhimishwa tarehe Juni 29.