Leandri wa Sevilia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Leandri wa Sevilia (Cartagena, leo nchini Hispania, 534 hivi - Sevilia, Hispania, 13 Machi 600 au 601) alikuwa askofu mkuu wa Sevilia ambaye kwa mahubiri na juhudi zake alifaulu kuingiza katika Kanisa Katoliki kutoka Uario Wavisigoti waliotawala Hispania na Ureno wa leo, kuanzia Hermengildi na Rekaredo, watoto wa mfalme.
Tangu zamani anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Machi[1] au 27 Februari.