Uhispania
nchi katika Ulaya Kusini-Magharibi / From Wikipedia, the free encyclopedia
Uhispania (Kihispania: España; Kiingereza: Spain) ni nchi ya Ulaya ya kusini-magharibi. Imepakana na Ufaransa, Andorra, Ureno na eneo la Kiingereza la Gibraltar.
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: Plus Ultra (Kilatini kwa "Mbele na zaidi") | |||||
Wimbo wa taifa: Marcha Real au Marcha Granadera | |||||
Mji mkuu | Madrid 40°26′ N 3°42′ W | ||||
Mji mkubwa nchini | Madrid | ||||
Lugha rasmi | Kihispania(1) | ||||
Serikali Mfalme Waziri Mkuu |
Ufalme wa kikatiba Felipe VI Pedro Sánchez | ||||
Kuungana kwa nchi Kungana kwa ndoa za wafalme Maungano Hali halisi Kisheria |
1516 1716 1812 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
504,782 km² (ya 50) 1.04% | ||||
Idadi ya watu - 2018 kadirio - 2001 sensa - Msongamano wa watu |
46.733.038 (ya 30) 40,847,371 92/km² (ya 112) | ||||
Fedha | Euro (€)(2) (EUR ) | ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
CETKigezo:Footnote (UTC+1) CEST (UTC+2) | ||||
Intaneti TLD | .es | ||||
Kodi ya simu | +34
- | ||||
Kigezo:Fnb Majimbo ya kujitawala ya Hispania yanatumia lugha za: Kikatalunya/Kivalencia, Kibaski na Kigalicia pamoja na Kihispania. Katika Bonde la Val d'Aran lahaja ya Kiarani ya lugha ya Kioksitani ni lugha rasmi pamoja na Kihispania; Kigezo:Fnb Hadi 1999: Peseta Kigezo:Fnb Ispokuwa Visiwa vya Kanari |
Kuna pwani ndefu ya Bahari ya Mediteranea na pia ya Atlantiki.
Uhispania bara ni sehemu kubwa ya rasi ya Iberia. Visiwa vya Baleari kwenye Mediteranea na Visiwa vya Kanari katika Atlantiki pamoja na miji ya Afrika ya Kaskazini Ceuta na Melilla ni sehemu za Uhispania.
Mji mkuu ni Madrid ambayo ni pia mji mkubwa wa nchi.
Eneo la nchi ni km² 505,990 nalo lina wakazi 47,450,795 (sensa ya mwaka 2020).
Mfalme Felipe VI amevaa taji mwaka 2014, akishika nafasi ya baba yake Juan Carlos I, anayeheshimiwa sana kwa sababu aliongoza taifa katika mabadiliko ya kutoka udikteta wa jenerali Francisco Franco kuelekea demokrasia. Hasa tendo la mfalme la kuzuia mapinduzi wa kijeshi linakumbukwa sana.
Muundo wa serikali ni Ufalme wa Kikatiba, hivyo kisheria madaraka ya mfalme ni madogo.
Utawala umo mikononi mwa serikali inayochaguliwa na bunge linaloitwa "Las Cortes likichaguliwa kwa kura za kidemokrasia.