Kikucha (Regulus)
Ndege wadogo wa jenasi Regulus, familia Regulidae / From Wikipedia, the free encyclopedia
Vikucha ni ndege wadogo sana wa jenasi Regulus, jenasi pekee ya familia Regulidae. Spishi za jenasi Sylvietta zinaitwa vikucha pia. Vikucha wa Regulus ni kijanikijivu wenye utosi njano au mwekundu. Katika Afrika wanatokea kutoka Maroko mpaka Tunisia na kisiwa cha Tenerife ndani ya misitu ya misonobari. Wanatokea pia Ulaya, Asia na Amerika ya Kaskazini. Hula wadudu ambao huwakamata juu mitini. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe kwa vigoga na kuvumwani lililoning'iniza mwishoni kwa tawi la juu la msonobari. Jike huyataga mayai 7-12.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kikucha | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kikucha utosi-dhahabu | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Spishi 7: | ||||||||||||||||
Funga