Yusta na Rufina
From Wikipedia, the free encyclopedia
Yusta na Rufina (Sevilia, Hispania, 268 na 270 - Sevilia, 287) walikuwa dada na mdogo wake waliouawa kwa sababu ya imani ya Kikristo.
Kisha kukamatwa na gavana Diogeniano, waliteswa kikatili na kuachwa bila chakula gerezani; ndipo alipofariki Yusta[1]. Rufina alizidi kukiri imani yake hadi alipovunjwa shingo kwa sababu hiyo[2].
Tangu kale wanaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.