Pio wa Pietrelcina
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pio wa Pietrelcina (25 Mei 1887 - 23 Septemba 1968) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa Ndugu Wadogo Wakapuchini.
Kwa miaka 50 katika konventi ya San Giovanni Rotondo alijitosa kuongoza kiroho waumini na kupatanisha watubu pamoja na kushughulikia kwa upendo maskini wa kila aina.
Alivumilia kishujaa kupingwa na kudhulumiwa, lakini pia aliheshimiwa na umati wa watu, kutokana na karama zake za pekee na wingi wa miujiza iliyoshuhudiwa nao.
Alimaliza maisha yake akiwa amelinganishwa vizuri ajabu na Yesu msulubiwa [1].
Mwaka 2002 alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mtakatifu: sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 23 Septemba, siku ya kifo chake[2].