Pasaka ya Kiyahudi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pasaka ya Kiyahudi (pia Passah au Pessah; Kiing. Passover) ni kati ya sikukuu muhimu zaidi za dini ya Uyahudi. Sikukuu hiyo inakumbuka Wanaisraeli walivyotoka katika utumwa walimokuwemo huko Misri.
Pasaka ya Kiyahudi imekuwa na athira kubwa juu ya sherehe ya Pasaka ya Kikristo kuhusu tarehe, liturujia na desturi mbalimbali.