Liturgia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Liturgia (pia: liturujia na liturugia; kutoka Kigiriki λειτουργια, leiturgia, yaani huduma kwa umati wa watu) ni utaratibu wa ibada hasa katika Kanisa la Kikristo.
Wakati mwingine neno hili linatumika pia kwa muundo au utaratibu wa sala katika dini mbalimbali.
Kwa kawaida liturgia inamaanisha utaratibu maalumu unaoweka mpangilio wa sala, nyimbo, masomo na sherehe nyingine wakati wa ibada.
Taratibu zinatofautiana kulingana na imani, teolojia, historia na utamaduni wa wahusika.
Hivyo ndani ya Ukristo kuna taratibu mbalimbali ambazo matawi yake makuu ni:
- liturgia ya Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki
- liturgia ya Wakatoliki wanaofuata mapokeo ya Roma
- liturgia ya madhehebu ya Uprotestanti wa asili (Walutheri, Waanglikana, Waprebiteri n.k.), tofauti na ubunifu wa yale ya Wapentekoste n.k.
Kiini cha liturgia ya Kikristo ni zile ibada zilizoanzishwa na Yesu mwenyewe, hasa ekaristi.