Panonia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Panonia (kwa Kilatini Pannonia) ilikuwa jimbo la Dola la Roma kuanzia mwaka 9 KK hadi 433. Eneo lake lilipakana na milima ya Alpi upande wa magharibi na mto Danubi upande wa kaskazini na mashariki. Leo hii eneo lake lakaliwa na Hungaria ya magharibi, Burgenland ya Austria na sehemu za Kroatia, Serbia na Slovenia. Wakati wa Roma ya kale jimbo liligawiwa mara mbili na mwaka 433 lilikabidhiwa kwa mfalme Attila wa Wahunni.