Nyasi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nyasi ni kundi la mimea inayofunika udongo; nyasi zilizo nyingi si kubwa sana lakini aina kama mianzi hufikia urefu wa miti. Kibiolojia hujumlishwa katika familia ya Poaceae au Gramineae.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Nyasi | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Nyasi | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Nusufamilia 12
|
Funga
Nyasi nyingi huwa na mizizi mirefu inayoshika ganda la juu la ardhi hivyo kuzuia au kupunguza mmomonyoko wa udongo. Kiekolojia aina za nyasi zimezoea mazingira tofauti kabisa kati ya kanda za joto hadi kanda za baridi sana. Wakati wa baridi au ukame majani juu ya ardhi hukauka hata kupotea kabisa lakini mizizi ina uwezo wa kulala muda mrefu na kusubiri mvua au halijoto ya juu zaidi.