Milki ya Kiptolemaio
From Wikipedia, the free encyclopedia
Milki ya Kiptolemaio (kwa Kigiriki: Πτολεμαϊκὴ βασιλεία, ptolemaaike basileia)[1] ulikuwa dola katika Misri na sehemu za Mashariki ya Kati kuanzia mwaka 305 KK hadi mwaka 30 BK. Ilitawaliwa na wafalme kutoka nasaba ya Waptolemaio waliokuwa Wagiriki na hivyo ufalme wao huhesabiwa kati ya milki za Kiheleni zilizotokea baada ya Aleksander Mkuu.