Korongo (Bovidae)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kwa maana tofauti ya neno hilo tazama Korongo (maana)
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Korongo | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Dume la korongo kusi (Hippotragus e. equinus) | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Spishi 3, nususpishi ??:
| ||||||||||||||||
Funga
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Korongo au kolongo ni spishi ya kawaida zaidi ya jenasi Hippotragus katika familia Bovidae. Spishi nyingine inaitwa palahala au mbarapi. Hawa ni wanyama wakubwa ambao wanatokea savana za Afrika zenye miti. Rangi ya madume ni kahawia hadi nyeusi, rangi ya majike ni kahawia. Kuna mabaka meusi na meupe kichwani, lakini hayaonekani sana kwa korongo buluu; tumbo ni jeupe. Dume na jike wana pembe ndefu zilizopindika kuelekea nyuma ambazo urefu wao unaweza kufika mita moja au zaidi lakini fupi zaidi kwa jike. Wanyama hawa hula manyasi marefu kiasi.