Yohane Gualberto
From Wikipedia, the free encyclopedia
Yohane Gualberto (995 hivi - 12 Julai 1073) alikuwa mmonaki wa Toscana, Italia ya Kati aliyeanzisha urekebisho wa Vallombrosa.
Kabla ya hapo alikuwa askari kutoka familia maarufu ya Visdomini. Ndugu yake alipouawa, alipaswa kulipa kisasi kwa kumuua muuaji. Alipompata, huyo alimpigia magoti na kunyosha mikono kama Yesu msalabani akimuomba msamaha. Ilikuwa siku ya Ijumaa Kuu. Hapo Yohane alitupa upanga wake na kumkumbatia.
Baada ya hapo alijiunga na monasteri ya Wabenedikto wa San Miniato.
Aliposhindana na abati na askofu wake wenye tabia ya usimoni, ambao yeye aliupiga vita, aliacha jumuia na mwaka 1036 alifika pamoja na wenzake kadhaa huko Vallombrosa [1].
Baada ya Papa kuthibitisha nia yao, shirika lilistawi sana.
Mwaka 1193 alitangazwa na Papa Celestino III kuwa mtakatifu.