Veronika Giuliani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Veronika Giuliani (Mercatello sul Metauro, Marche, Italia, 27 Desemba 1660 - Città di Castello, Umbria, Italia, 9 Julai 1727) alikuwa mmonaki wa urekebisho wa Wakapuchini wa Utawa wa Mt. Klara.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu bikira. Ingawa aliheshimiwa hivyo mara baada ya kufa, kesi ya kumtangaza rasmi ilicheleweshwa na uchunguzi wa maandishi yake marefu.
Papa Pius VII ndiye aliyemtangaza mwenye heri mnamo Juni 1804, halafu Papa Gregori XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 26 Mei 1839.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyofariki dunia[1] au kesho yake.