Vedasto wa Arras
From Wikipedia, the free encyclopedia
Vedasto wa Arras (pia: Vedastus, Vaast, Waast, Gaston, Foster; 453 – Arras, Pas-de-Calais, 540) alikuwa askofu wa mji huo (leo nchini Ufaransa) kwa miaka zaidi ya 40. Alikuwa ametumwa huko na Remi wa Reims wakati mji ulipokuwa umeangamizwa, akainjilisha mfalme Klovis akiingiza Wapagani wengi katika Kanisa Katoliki[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Februari[2].