Spishi adimu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Shishi adimuni spishi ambazo zimeandikwa na International Union for Conservation of Nature (IUCN) katika orodha maalumu yenye majina ya zile zinazoelekea kukoma duniani (Red List).
Mwaka 2012 orodha hiyo ilikuwa na spishi za wanyama 3079 na spishi za mimea 2655,[2] wakati mwaka 1998 zilikuwa 1102 na 1197 tu.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya asilimia 40 za spishi ziko hatarini.
Siku hizi nchi nyingi zina sheria za kuhifadhi spishi za namna hiyo, kwa kukataza, k.mf. uwindaji na uchomaji moto, au kwa kuunda maeneo maalumu hifadhi za taifa.
Pia kuna mikataba ya kimataifa iliyosainiwa na nchi zote au karibu zote kwa ajili hiyo.