Sozonti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sozonti (alifariki Soli/Pompeiopoli, leo Mersin, Kilikia, nchini Uturuki, 300 hivi) alikuwa mvulana mchungaji wa mifugo aliyejiunga na Ukristo.
Baada ya kubomoa sanamu kadhaa za miungu alifia dini yake wakati wa dhuluma ya kaisari Dioklesyano[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Sikukuu yake ni tarehe 7 Septemba[2].