Selulosi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Selulosi (kutoka neno la Kiingereza "cellulose"[1]) ni tishu iundayo sehemu kubwa ya miti na mimea mingine.
Kikemia inaundwa na sehemu nyingi za glukosi yenye fomula (C6H10O5)n zinazounganishwa kuwa molekuli ndefu (polima).
Selulosi inapatikana zaidi kwenye mimea ya rangi ya kijani na inatengeneza kiwambaseli cha mmea.
Selulosi haiwezi kuliwa na wanyama lakini spishi kadhaa, kama vile mchwa na ng'ombe, hutunza bakteria katika matumbo yao wanaovunja molekuli za selulosi kwa sehemu ndogo zaidi zinazoweza kumeng’enywa.