Nchi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nchi kwa maana ya msingi ni Dunia, hasa sehemu yake isiyofunikwa na bahari. Mara nyingi zaidi inataja sehemu maalumu iliyogawanyika kisiasa kwa mipaka na kutajawa kwa jina lake. Kwa maana hiyo ya kawaida nchi ni kitengo cha kisiasa katika eneo maalumu. Kwa kawaida nchi ni pia dola, lakini ziko pia nchi ambazo ni sehemu ya dola kubwa zaidi.
Katika baadhi ya matumizi inaashiria majimbo na vitengo vingine vya kisiasa[1][2][3] ilihali katika mengine inahusu tu majimbo [4]. Si nadra kwa taarifa ya ujumla au machapisho ya takwimu kuchukua ufafanuzi mpana wa neno hili kwa makusudi kama maonyesho na ulinganifu.[5][6][7][8][9]
Baadhi ya maeneo yaliyokuwa zamani nchi au pia madola ya pekee na baadaye sehemu za dola kubwa zaidi, bado zinajulikana kama "nchi" hasa kama yametunza kiasi cha utamaduni wao, kama vile Uingereza, Uskoti na Welisi - katika Ufalme wa Muungano.[10][11][12][13] Kihistoria, nchi za Umoja wa zamani wa Kisovyeti na Yugoslavia zilikuwa nyingine za namna hiyo. Majimbo ya zamani kama Bavaria (sasa ni sehemu ya Ujerumani) na Piemonte (sasa ni sehemu ya Italia) yangekuwa si kawaida kujulikana kama "nchi" katika Kiingereza cha kisasa.
Kiwango cha uhuru wa nchi zisizo mataifa inatofautiana sana. Baadhi ni mali ya mataifa, kwani mataifa kadhaa yana maeneo yanayoyategemea ya ng'ambo (kama vile Visiwa vya Virgin vya Uingereza, Saint Pierre na Miquelon, na Samoa ya Marekani), yenye eneo na raia tofauti na yao wenyewe. Maeneo tegemezi kama hayo wakati mwingine yanatajwa pamoja na mataifa huru kwenye orodha ya nchi, na yanaweza kuchukuliwa kama "nchi ya asili" katika biashara ya kimataifa, kama Hong Kong ilivyo. Baadhi ya nchi zimegawanywa kati ya madola kadhaa, kama vile Korea na Kurdistan.