Mzingo antaktiki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mzingo antaktiki (kwa Kiingereza: Antarctic circle) ni mstari wa kudhaniwa kwenye uso wa Dunia kwa latitudo ya kusini ya 66° 33' 50 hivi[1]. Umbali wake na ncha ya kusini ni takriban kilomita 2,600, umbali kutoka ikweta km 15,996.
Kinyume chake ni mzingo aktiki upande wa kaskazini ya Dunia.