Mlipuko wa homa ya mafua wa 1918
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mlipuko wa homa ya mafua wa 1918 (unaojulikana pia kama Spanish Flu) ulikuwa pandemia ya homa ya mafua iliyotokea kwenye mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Ulidumu miaka mitatu, kuanzia Januari 1918 hadi Desemba 1920. [1] Takriban watu milioni 500[2] waliambukizwa duniani kote ilhali wakati ule idadi ya watu duniani ilikuwa milioni 1,800 tu.