Mwanzi (nyasi)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mwanzi ni jina la spishi nyingi za nyasi ndefu zinazoweza kuonekana kama miti. Mianzi yote huwa na shina ya aina ya ubao.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Mwanzi (Bambuseae) | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Msitu wa mianzi huko Japani | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Makabila 3:
|
Funga
Mianzi hupatikana kiasili katika Afrika, Amerika na Asia lakini inastawi pia ikipandwa Ulaya.
Urefu wa spishi kubwa hufikia kina cha mita 40. Inaweza kukua zaidi ya mita 1 kila siku lakini kwa kawaida ni sentimita 3-5 kwa siku.
Shina la mianzi huwa na umbo la bomba na unene wake ni hadi sentimita 30. Shina hugawiwa na vifundo. Kila kifundo kina chipukizi na machipukizi yanaweza kuendelea kuota matawi.