Magdalena wa Canossa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Magdalena wa Canossa (Verona, Italia, 1 Machi 1774 - Verona, 10 Aprili 1835) alikuwa mwanamke aliyejinyima utajiri wake wote akaanzisha mashirika ya Mabinti wa Upendo (Wakanosa) na Wana wa Upendo (Wakanosa) kwa ajili ya malezi ya Kikristo ya vijana.
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu mwaka 1988.