Lusiano wa Antiokia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lusiano wa Antiokia (labda Samosata, leo Samsat, Uturuki, 240 hivi – labda Nikomedia, 7 Januari 312) alikuwa padri mwanateolojia ambaye alijulikana pia kwa uadilifu wake mkubwa na hatimaye alifia dini ya Ukristo kwa kukatwa kichwa au kwa kuachwa afe njaa[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Januari[2][1] au 15 Oktoba.