Koloni za Ufaransa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Koloni za Ufaransa zilikuwa maeneo yaliyodhibitiwa na Ufaransa kutoka karne ya 17 hadi mwishoni mwa miaka ya 1960. Maeneo machache ambayo hayajapata uhuru yamekuwa sehemu za Jamhuri ya Ufaransa kama maeneo ya ng'ambo ya Ufaransa yenye hadhi ya mikoa na wananchi wana haki zote za raia wa Ufaransa na Umoja wa Ulaya.
Wanahistoria hutofautisha mara nyingi awamu ya kwanza na awamu ya pili ya ukoloni wa Ufaransa.