Katerina wa Siena
Mtakatifu wa Dominika wa Italia (1347-1380 / From Wikipedia, the free encyclopedia
Katerina Benincasa wa Siena (Siena, Italia, 25 Machi 1347 - Roma, Italia, 29 Aprili 1380) alikuwa mwanamke mwenye vipaji na karama za pekee aliyemfuata tangu ujanani Yesu Kristo ili kulingana naye katika familia ya kiroho iliyoanzishwa na Dominiko Guzman, akijitahidi kumfahamu Mungu ndani yake na kujifahamu ndani ya Mungu.
Ingawa hakusoma, alishika nafasi muhimu katika historia ya Kanisa, akisababisha wongofu na urekebisho, na katika historia ya Italia, akileta amani wakati wa vita na fujo nyingi za siasa.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu bikira na mwalimu wa Kanisa.
Kutokana na umuhimu wake katika historia ya Kanisa na ya jamii ni msimamizi (pamoja na wengine) wa Italia (kwa uamuzi wa Papa Pius XII mwaka 1939) na wa Ulaya (kwa uamuzi wa Papa Yohane Paulo II mwaka 1999).