Karolo wa Sezze
From Wikipedia, the free encyclopedia
Karolo wa Sezze (Sezze, leo katika wilaya ya Latina, Italia, 19 Oktoba 1613 - Roma, 6 Januari 1670), alikuwa bradha wa shirika la Ndugu Wadogo Wareformati aliyeandika vizuri sana kuhusu maisha ya kiroho.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.[1]
Alitangazwa kwanza mwenye heri na Papa Leo XIII mwaka 1882, halafu mtakatifu na Papa Yohane XXIII tarehe 12 Aprili 1959.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake, 6 Januari, au kesho yake[2].