Ghat ya Magharibi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Milima ya Ghat ya Magharibi ni eneo la milima inayoenea katika urefu wa km 1,600 sambamba na pwani ya magharibi ya Bara Hindi, kupitia majimbo ya Kerala, Tamil Nadu, Karnataka, Goa, Maharashtra na Gujarat[1].
Ni eneo lililoandikishwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia likiwa kati ya vitovu vya bioanwai[2]. Kuna idadi kubwa ya spishi za wanyama na mimea ambayo inapatikana nchini Uhindi pekee.