Fransisko wa Sales
From Wikipedia, the free encyclopedia
Fransisko wa Sales (Thorens-Glières, leo nchini Ufaransa, 21 Agosti 1567 - Lyon, Ufaransa, 28 Desemba 1622) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki kwa jimbo la Geneva (Uswisi).
Akijumlisha ndani mwake matunda bora ya karne XVI, ni kati ya watu muhimu zaidi katika Urekebisho wa Kikatoliki na katika teolojia ya maisha ya kiroho.
Mchungaji halisi, alirudisha katika Kanisa Katoliki Waprotestanti wengi, na kuwafundisha kwa maandishi yake Wakristo wamheshimu na kumpenda Mungu. Pamoja na Yoana Fransiska wa Chantal alianzisha shirika la Ziara.
Kwa ajili hiyo anaheshimiwa kama mtakatifu na mwalimu wa Kanisa. Pia kama msimamizi wa waandishi wa habari, watunzi na wanafasihi, magazeti ya Kikatoliki na mabubu-viziwi.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 24 Januari[1].