Felix wa Cantalice
From Wikipedia, the free encyclopedia
Felix wa Cantalice ndilo jina la kitawa la Felice Porri (Cantalice, Rieti, Italia, 1515 hivi - Roma 18 Mei 1587) aliyekuwa bruda wa urekebisho wa Ndugu Wadogo Wakapuchini, mwenye unyofu na ugumu wa maisha wa ajabu, ambaye kwa miaka 40 alifanya kazi ya ombaomba[1] kwa ajili ya watawa wenzake na kwa ajili ya fukara akieneza upendo na amani mjini Roma [2] [3].
Alitangazwa mwenye heri tarehe 1 Oktoba 1625 na mtakatifu tarehe 22 Mei 1712, wa kwanza wa shirika hilo kutangazwa hivyo.