Damian de Veuster
From Wikipedia, the free encyclopedia
Damian de Veuster (3 Januari 1840 - 15 Aprili 1889) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa Shirika la Mioyo Mitakatifu maarufu kama Picpus. Kwa miaka mingi alikuwa mmisionari katika kisiwa cha Molokai (Hawaii), alipojitosa kutumikia wagonjwa wengi wa ukoma waliotengwa huko hata akaambukizwa nao.
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri mwaka 1995, na Papa Benedikto XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 11 Oktoba 2009.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe ya kifo chake[1] au 10 Mei.