Bilioni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bilioni (kutoka Kiingereza "billion"[1][2]) ni namba ambayo inamaanisha milioni elfu moja na kuandikwa 1,000,000,000.
Inafuata 999,999,999 na kufuatwa na 1,000,000,001.
Inaweza kuandikwa pia kifupi 1 × 109.
Kiambishi awali giga kinatumika pia kumaanisha mara 1,000,000,000, ingawa katika lugha nyingine nyingi neno linalofanana na "bilioni" linamaanisha milioni milioni (1,000,000,000,000).