Bernodi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bernodi (pia: Bernold, Bernulf, Benno au Bernulphus; alifariki Utrecht, leo nchini Uholanzi, 19 Julai 1054) alikuwa askofu wa mji huo tangu mwaka 1027 hivi.
Alikomboa makanisa na monasteri kutoka mamlaka ya watawala, aliyanzisha makanisa mapya mengi na kufanya monasteri zifuate urekebisho wa Cluny [1].