Bernardo wa Clairvaux
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bernardo wa Clairvaux (Fontaine-lès-Dijon, Ufaransa, 1090 - Ville-sous-la-Ferté, Ufaransa, 20 Agosti 1153) alikuwa padri, abati na mwenezaji mkuu wa urekebisho wa Citeaux wa shirika la Benedikto wa Nursia.
Aliongoza kwa hekima wamonaki wenzake katika njia za amri za Mungu kwa maisha, mafundisho na mifano yake mwenyewe. Lakini pia alisafiri kote Ulaya ili kurudisha amani na umoja akaangaza Kanisa lote kwa maandishi na mahubiri yake motomoto[1].
Aliitwa “Babu wa mwisho” kwa sababu alitetea na kustawisha teolojia ya mababu wa Kanisa wakati wa kujitokeza teolojia mpya ya shule.
Ndiye mtu muhimu zaidi wa karne ya 12 katika Kanisa Katoliki, ambalo linamheshimu kama mtakatifu (alivyotangazwa na Papa Alexander III mwaka 1174) na mwalimu wa Kanisa (alivyotangazwa na Papa Pius VIII mwaka 1830).
Ni msimamizi wa wakulima.