Bendera ya Tanzania
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bendera ya Tanzania ni ya mstatili unaokatwa pembe kwa pembe na kanda nyeusi yenye milia za njano kandokando[1].
Pembetatu ya juu ina rangi ya majani, pembetatu ya chini ni ya buluu.
Matumizi ya bendera inahifadhiwa chini ya sheria ya "The National Flag and Coat of Arms Act, 15-1971"[2].