Assisi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Assisi (inatamkwa Asizi) ni mji wa Italia, mkoa wa Umbria, wilaya ya Perugia. Wakazi wake ni 26.946 (2007).
Ukweli wa haraka Nchi, Mkoa ...
Assisi | |
Nchi | Italia |
---|---|
Mkoa | Umbria |
Wilaya | Perugia |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 26,946 |
Tovuti: http://www.comune.assisi.pg.it/ |
Funga
Ni maarufu hasa kwa kuwa ndiko alikozaliwa mtakatifu Fransisko (1182-1226), shemasi aliyeanzisha utawa wenye matawi mbalimbali ambao ni mkubwa kuliko mashirika yote ya Kanisa Katoliki.
Miaka hiyohiyo huko walizaliwa pia kaisari Federiko II, Klara wa Asizi na Anyesi wa Asizi.
Baadaye tena hukohuko alizaliwa mtakatifu mwingine, Gabriele wa Mama wa Mateso.
Sehemu mbalimbali za mji huo zimo katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO.