Aristoteli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Aristoteli (kwa Kigiriki Αριστοτέλης, Aristotelēs; pia: Aristo; 384 KK - 7 Machi 322 KK) alikuwa mwanafalsafa muhimu wa ustaarabu wa Ugiriki ya Kale.
Pamoja na Plato huhesabiwa kati ya wanafalsafa muhimu zaidi katika utamaduni wa magharibi. Aristoteli alikuwa mwalimu wa Aleksander Mkuu kabla huyu hajawa mfalme.
Alichangia sehemu kubwa sana katika elimu ya sayansi na falsafa. mawazo na ugunduzi wake umewachochea watu na maandishi yake yametafsiriwa na kusomwa na watu wengi sana. [1]
Aristoteli aliandika kuhusu sanaa, nyota, biolojia, maadili, lugha, sheria. Zamani watu wa Ulaya walifuata mafundisho ya Aristoteli. Mwanateolojia mashuhuri wa Roma Thomas Aquinas alitumia sana maandishi ya Aristoteli.