Andalusia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Andalusia (kwa Kihispania: Andalucía) ni jimbo la kujitawala (Kihisp.: comunidade autónoma) la Hispania katika kusini ya rasi ya Iberia. Mji mkuu ni Sevilla. Katika historia ni sehemu ya Hispania iliyowahi kutwaliwa na iliyotawaliwa kwa karne nyingi zaidi na Waarabu Waislamu.