Usiku wa roho
From Wikipedia, the free encyclopedia
Usiku wa roho ni istilahi ya maisha ya kiroho iliyotumika hasa katika Kanisa Katoliki kwa kufuata mang'amuzi na mafundisho ya Yohane wa Msalaba. Kadiri yake, Mkristo aliyeendelea katika maadili na usikivu kwa vipaji vya Roho Mtakatifu anahitaji kupatwa na utakaso huo kutoka kwa Mwenyezi Mungu ili kuwa tayari kwa hatua ya muungano.