Shirika la ndege
From Wikipedia, the free encyclopedia
Shirika la ndege ni kampuni inayotoa huduma ya usafiri wa anga wa kiraia kwa abiria na mizigo. Mashirika ya ndege hutumia ndege kutoa huduma hizi. Kawaida, mashirika haya hupewa leseni na idara husika ya serikali.
Mashirika ya ndege hutofautiana kwa ukubwa, toka mashirika ya ndege madogo ya safari za ndani na mashirika makubwa ya safari za kimataifa. Mnamo 2019 shirika la ndege kubwa kuliko yote duniani ni American Airlines Group.