Nyota nova
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nyota nova (lat. stella nova kwa maana ya "nyota mpya", ing. nova) ni ongezeko la ghafla la mwangaza wa nyota. Ilhali idadi kubwa za nyota hazionekani kwa macho matupu ongezeko hili linatokea mara nyingi kama "nyota mpya" angani inayoweza kung'aa sana hata kushinda nyota zote nyingine. Hivyo inaonekana kwa muda tu na kupotea tena kwa mtazamaji asiye na darubini.