Ngoma (ala ya muziki)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ngoma ni ala ya muziki inayopigwa kwa mkono au kwa fimbo.
Ngoma hufanywa kwa kukaza utando juu ya mzinga. Utando mara nyingi ni wa ngozi na siku hizi pia plastiki. Mzinga unaweza kufanywa kwa ubao, metali, udongo uliofinyangwa au chochote kile kinacholeta nafasi yenye kuta na uwazi ambako utando unafungwa.
Ngoma ni ala ya jadi katika Afrika na pia sehemu nyingine za dunia. Mara nyingi zilitengenezwa kwa kutumia kipande cha shina la mti na kuondoa ubao wa katikati halafu kukaza ngozi juu yake.