Neema
From Wikipedia, the free encyclopedia
Neema ni jambo lolote jema ambalo binadamu anapata katika maisha yake.
Neno hilo kwa Kiswahili ni pana, lenye maana mbalimbali, kama vile mema ya kiroho na ya kiuchumi, lakini zote zinaelekeza kumfikiria Mungu kama asili yake kuu. Ni huruma ya Mungu kwa wanadamu inayoambatana na baraka.
Teolojia katika dini mbalimbali inatumia neno hili kadiri ya imani yake.
Kwa namna ya pekee neno linatiwa mkazo katika Ukristo unaosisitiza kwamba mambo yote ni neema (kwa Kigiriki: χάρις, kharis; kwa Kilatini: gratia, yaani deso, kitu cha bure).
Hata hivyo madhehebu yake yanatofautiana sana katika kutafsiri tamko hilo.