Maria wa Yesu Ekaristi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Maria wa Yesu Ekaristi (kwa Kihispania: María de Jesús Sacramentado; jina la awali: Maria Navidad Venegas de la Torre, Zapotlanejo, Jalisco, 8 Septemba 1868 - Guadalajara, 30 Julai 1959) alikuwa mwanamke Mkristo wa Meksiko aliyeanzisha shirika la Mabinti wa Moyo Mtakatifu wa Yesu.
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 22 Novemba 1992, tena mtakatifu tarehe 21 Mei 2000.