Mamba (mnyama)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mamba au ngwena ni spishi kubwa za reptilia za oda Crocodilia. Mamba wanaishi majini na hupatikana maeneo mengi ya kitropiki katika Afrika, Asia, Australia na Amerika. Mamba hupenda kuishi katika maji baridi kama vile maziwa, mito, ardhi tepe-tepe. Mamba hula hasa wanyama wenye uti wa mgongo kama vile samaki, reptilia na mamalia na wakati mwingine hata wale wasio na uti wa mgongo kama vile jamii ya konokono , moluski na kaasi kutegemeana na aina yao hasa. Mamba bado ni mlolongo wa viumbe wa kale na husemekana kuwa wamekadiriwa kidogo mno, tangu enzi zile za mirosana.
Mamba | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mamba wa Afrika | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Familia 3:
| ||||||||||||
Inaaminika spishi za mamba zilianza katika ukoo wa wanyama waliokuwa karibu na dinosauri lakini hazikuangamizwa katika tukio lililosababisha kutoweka kwa masauri miaka milioni 65 iliyopita. Mamba wamepona na kuepuka matukio mengi sana ya kutoweka.