Lava
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kwa matumizi mengine ya jina hili angalia lava (volkeno)
Lava (kutoka neno la Kiingereza larva ambalo lina asili ya Kilatini; pia bombwe) ni mtoto wa mdudu au wa mmojawapo wa invertebrata, amfibia au samaki katika hatua za awali za ukuaji wake.
Lava wa wadudu kadhaa wana majina ya pekee:
- jana ni lava wa nyuki
- buu na funza ni lava wa nzi na mbawakawa fulani
- kiluwiluwi ni lava wa mbu
- kiwavi ni lava wa kipepeo
- tunutu ni lava wa nzige
Kuna pia amfibia wanaopita hali ya lava. [[Ndubwi au kiluwiluwi ni lava wa chura.
Lava wa spishi mbalimbali huendelea kupitia hali ya pupa kabla ya kuendelea katika ngazi ya mwisho wa mabadiliko ya maumbile metafofosi.