La Amistad
From Wikipedia, the free encyclopedia
La Amistad (neno la Kihispania kwa "Urafiki") ilikuwa jahazi yenye milingoti miwili katika karne ya 19, iliyomilikiwa na Mhispania kwenye kisiwa cha Kuba, wakati ule koloni la Hispania.
Ilijulikana mnamo Julai 1839 kwa uasi wa wafungwa Waafrika waliomwua nahodha na kuteka chombo hicho. Mbele ya pwani ya Marekani walikutana na manowari ya Kimarekani iliyowakamata. Katika kesi zilizofuata mbele ya mahakama mbalimbali madai ya Hispania ya kuwarudisha Kuba kama watumwa yalikataliwa. Kesi ya La Amistad ilikuwa na ushawishi mkubwa kwa harakati ya kupinga utumwa Marekani.
Uasi huo, pamoja na kesi zake, ni msingi wa vitabu mbalimbali pamoja na filamu "Amistad" iliyoongozwa na Steven Spielberg kwenye mwaka 1997.