Kunguni-mgunda
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kunguni-mgunda ni wadudu wadogo hadi wakubwa kiasi wa oda ya chini Pentatomomorpha katika oda Hemiptera ya nusungeli Pterygota (wenye mabawa) ambao wana mabawa ya mbele yaliyo nusu magumu na nusu kama kiwambo. Takriban wadudu hao wote hufyonza utomvu wa mimea, matunda au mbegu, lakini spishi nyingine hula kuvu na nyoga au wadudu wadogo. Spishi fulani huitwa visulisuli pia.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kunguni-mgunda | ||||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kisulisuli mraba-mweusi (Dysdercus nigrofasciatus) | ||||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||||
Familia za juu 5:
| ||||||||||||||||||||
Funga
Mifano ya wadudu hao ni kunguni-ngao (familia Pentatomidae), kunguni-bapa (familia Aradidae), kunguni-mbegu (familia Lygaeidae na Rhyparochromidae) n.k.