Emma wa Lesum
From Wikipedia, the free encyclopedia
Emma wa Lesum (au Hemma au Imma wa Stiepel au wa Ludger; 975-980 ā 3 Desemba 1038) alikuwa mwanamke wa ukoo Immedinger, uliotawala kaskazini mwa Ujerumani. Aliolewa na kuzaa mtoto mmoja, halafu akafiwa mumewe.
Kutokana na matendo yake mema, tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake au tarehe 17 Aprili.