Ambohimanga
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ambohimanga ni jina la mlima karibu na Antananarivo katika Madagaska. Katika karne ya 18 ilikuwa makao makuu ya sehemu ya wafalme wa Wamerina walioteka kutoka hapa sehemu nyingine za Imerina ikaendelea kuwa mahali pa makaburi ya wafalme wa Madagaska hadi mwaka 1897. Tangu mwaka 2001 imeandikishwa katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO.